TAMBUA AFYA YAKO. TUANGALIE MADHARA YA UZITO ULIOPITILIZA (Obesity). Uzito mkubwa wa kupindukia ni tatizo kubwa la kiafya katika maisha yetu ya kisasa. Uzito unapozidi kiwango ambacho kinahitajika kwa mtu husika kunachangia matatizo mengi ya kiafya. Kwa mujibu wa Takwimu zilizotolewa na shirika la afya duniani, zaidi ya watu bilioni 1.5 duniani wamezidisha uzito wa miili yao. Milioni 500 kati yao huwa na uzito wa kupindukia. Tatizo hili la UZITO uliopitiliza kuliko inavyohitajika kiafya huwa linaletwa na kuongezeka kwa kiwango cha mafuta mwilini. Njia rahisi inayokubalika ya kuweza kugundua kama mtu ni MZITO/MNENE kupita kiasi (Obese) inafahamika kama kipimo cha Body Mass Index (BMI). Vipimo hivi vya BMI ndio vinaweza kukujulisha kama unene ulionao unastahili kulingana na umri, urefu na...